Monday, December 22, 2014

LAKE RUKWA BASIN-HATARI YA KUKAUKA MAJI MWAKA 2022

Na Thompson Mpanji                                                  

WATAALAMU  wa maji wamebainisha kuwa  hadi kufikia mwaka 2022 wananchi wabonde la Ziwa Rukwa katika mikoa ya Mbeya na Rukwa watakuwa na upungufu mkubwa wa mahitaji ya maji kutokana na uharibifu mkubwa wa mazingira hii si habari njema hata kidogo kwa watanzania,wakati Serikali ya Tanzania inasema kufikia mwaka 2025 kila Mtanzania atakuwa na angalau unafuu wa maisha.

Kwa hivi sasa imekadiriwa kuwa mtu mmoja wa bonde la Ziwa Rukwa anatumia mita za ujazo 2250 kwa mwaka kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2002 ambapo idadi ya wakazi wa bonde hilo walikadiriwa kufikia 2,168,240 ambapo inakadiriwa kuwepo  na ongezeko la wakazi  mara mbili hadi kufikia  wakazi 4,525,652.

Tafiti zinasema kuwa kutokana na kuwepo kwa ongezeko kubwa la watumiaji wa maji mahitaji ya maji kwa mtu mmoja kwa mwaka yatapungua hadi kufikia mita 1500 za ujazo kiwango kinachodaiwa kuwa ni cha wastani kwa mujibu wa taarifa za kitaalamu za kimataifa.

Hicho ni kiwango cha wastani na kinadaiwa kuwa kikishuka chini ya hapo basi hali itakuwa mbaya sana kwa binadamu,wanyama na viumbe vyote vilivyo hai kwa maana watu wanazidi kuongezeka na hivyo mahitaji yanazidi kuongezeka lakini mazingira yanazidi kuharibiwa na hivyo maji yanapunguwa na hatimaye kukauka kabisa.

Wataalamu wa maji wanasema shughuli za binadamu kando kando ya mto zinatakiwa zianzie mita 250 kutoka ukingoni na Ziwa ni umbali ya mita 500 lakini sheria za hamashauri na Serikali za mitaa zinasema umbali ni mita kati ya 30 na 50 tu ebu angalia sheria hizo namna zinavyokinzana kwa hiyo jamii  imsikilize nani?.

Amini usiamini lakini ndivyo ilivyo kuwa kina cha maji cha Ziwa hilo kimepunguwa hadi kufikia mita mbili(mita 2)kwa mwaka 2006 na 2007 je kwa sasa kitakuwa kimefikia wapi kwani ukiangalia kwa macho tu Ziwalinaonekana kuzidi kurudi ndani na kwamba hali hiyo inatokana na  Ziwahilo kujaa matope na taka nyingi,lakini pia maji yamepunguwa kwa kiasi kikubwa kutoka usawa wa ardhi hadi kufikia mita zaidi ya 300 kuingia ndani ya Ziwa kwa mwaka huo.

Kwa ujumla Ziwa Rukwa lina umuhimu mkubwa kwa mahitaji ya binadamu na viumbe,mathalani ;Hifadhi za Taifa zilizopakana na Ziwa hilo kama Katavi,Rungwa,Rukwa na Lukwati zinategemea sana kipindi cha kiangazi kuendeleza unyevu na matumizi ya kurutubisha uoto wa asili.


Shughuli za usimamizi wa rasilimali za maji katika mabonde zipo kwa mujibu kwa mujibu wa sheria namba 42 ya mwaka 1974 na sheria ya marekebisho namba 10 ya mwaka 1981,lakini je zinasaidia vipi katika kutunza na kuhifadhi mazingira ya bonde la Ziwa Rukwa na kulinusuru na hatari ya kukauka na kuleta madhara makubwa kwa binadamu na viumbe  vilivyo hai vinavyotegemea ikolojia ya Ziwa hilo?.

Wizara  ya maji kwa kushirikiana na wadau mbalimbali  wameamua kuketi kwa muda wa siku mbili  katika ukumbi wa mikutano wa Mkapa,uliopo Soweto,jijini Mbeya  wakishirikiana na watumiaji wa maji  katika Mikoa mitano  inayopitiwa bonde la Ziwa Rukwa  ambayo Mbeya,Katavi,Rukwa,Tabora na Singida.

Ofisa wa maji  bonde la Ziwa Rukwa,Florence Mahay amesema  wameamua kukutana na wadau mbalimbali waliopo ndani ya bonde hilo ili kupokea taarifa ya  utafiti shirikishi wa matumizi bora  ya rasilimali maji   na kuangalia njia mbadala ya kuhakikisha wanafanya juhudi za kulinusuru bonde hilo ingawa kwa mujibu wa taarifa za watafiti  kuwa  kwa sasa kuna kiasi kikubwa cha maji.

"Kwa ujumla kuna uchafuzi mkubwa  na uharibifu wa mazingira katika bonde la Ziwa Rukwa,watu wanalima kando ya Ziwa na mito,wafugaji wanachungia mifugo yao  katika maeno hayo,ukataji wa miti  ovyo katika bonde,matumizi mabaya ya kemikali katika uchenjuaji wa madini na hasa aina ya dhahabu na masuala shughuli nyingine za kibinadamu zinachangia kuhatarisha ukosefu wa maji,"amesema.


Mwandishi wa  makala hii amezungumza na  Ofisa mipango  wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Fosfan Nsuli  ambapo ameelezea hofu yake  ya kutoweka kwa wanyamapori  waliopo katika Bonde la Mto Katuma  katika  hifadhi ya Katavi ambapo wanyama kama Viboko na mamba  wakiwa na hali mbaya  kutokana na kujikuta wakiwa wamerundikana katika bwawa moja lenye matope huku wakijisaidia haja kubwa na ndogo humo humo.


Hata hivyo Profesa Japhet Kashaigile kutoka Chuo kikuu cha Sokoine  amesema kuwa warsha  hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa jamii  kujuwa umuhimu wa kutunza rasilimali maji kwa ajili ya mazingira  huku Prof Aris Georgakakos  kutoka Taasisi ya Gorgia institute of Technology  akitoa wito kwa jamii kuzingatia yale waliyowaeleza kwa afya ya maisha yao.

"Ni vema wananchi wakazingatia kile tulichowafundisha  katika kuhakikisha  wanatunza na kuhifadhi mazingira,maji yatakuwa mengi,safi na salama  na radha nzuri,na huu ni utafiti wa awali tu lakini tunaendelea na utafiti  ili tuweze kubaini kiasi cha maji kilichopo ingawa kwa sasa maji ni mengi na ya kutosha,"amesema Aris.

Profesa huyo amesema kuwa  utafiti wanaoendelea nao utabaini  mahitaji ya maji kwa wananchi wanaoishi katika mikoa mitano  na watakuja kukaa tena na kuzungumza tena na watumiaji na wadau ikiwa ni njia ya ushirikishwaji jamii kuhusu matumizi bora ya rasilimali maji.

Mwisho.


Sunday, November 2, 2014

Watumiaji holela wa maji katika kilimo cha umwagiliaji wa zao la Mpunga,wilayani Mbarali katika bonde la Rufiji ni wengi kuliko wenye vibali halali,wanasiasa wadaiwa kukwamishamikakati ya utuzaji na uhifadhi wa mazingira pamoja na usimamizi wa rasilimali maji

Bwawa la Mtera lilivyokauka kwa sasa

Bwawa la Mtera  likionekana na  maji yanapofikia kwa sasa

Juu kipande cha picha kushoto kinaonesha  maji yalivyokauka,ambapo picha  ya kulia  juu na kushoto chini  hali mbaya  ya  maji ambapo picha ya chini kulia tembo  wakiwa na kiu ya maji wakisaka maji  kwa kuchimba  chini

Miundo mbinu ya kienyeji inavyoathiri rasilimali maji

Miundo mbinu bora ni muhimu katika  usimamizi wa matumizi  ya rasilimali maji kama inavyoonekana pichani

Miundo mbinu isiyozingatia utaalamu  ni kikwazo kikubwa katika usimamizi wa rasilimaali maji kama pichani inavyoonekana  wataalamu  wakiangalia mmoja wa wakulima aliyeamua kukinga  maji yasiendelee katika njia yake ya asili,wilayani Mbarali.

Kuhama kwa mkondo wa  mto kunatokana na uwepo wa mifereji holela kama picha inavyoonesha katika Mto Chimala,wilayani Mbarali.

Kilimo cha vinyungu  na matumizi  mabaya  ya maji kwenye shamba lililovunwa ni kikwazo





Sunday, August 11, 2013

NANE NANE MBEYA

MFANYAKAZI WA KAMPUNI YA TANSEED LTD INAYOSAMBAZA MBEGU ZA AINA MBALIMBALI AKIWA NJE YA BANDA LA KAMPUNI  HIYO KATIKA PICHA TOFAUTI WAKATI WA MAADHIMISHO YA SIKU KUKUU YA WAKULIMA NANE ILIYOFANYIKA KIKANDA KATIKA VIWANJA VYA JOHN MWAKANGALE,MKOANI MBEYA


BAADHI YA WAJASILIAMALI KUTOKA WILAYANI CHUNYA WAKIONESHA UTAALAMU WAO WA KUTENGENEZA VIATU,SANDALS,POCHI NA BIDHAA MBALIMBALI KWA KUTUMIA NGOZI YA NG'OMBE ILIYOSINDIKWA KITAALAMU KAMA WANAVYOONEKANA PICHANI WAKIWA KATIKA BANDA LAO WAKATI WA MAONYESHO YA NANE NANE,MKOANI MBEYA.

BLOG HII ITAKUWA INATOA HABARI MBALIMBALI ZA UTUNZAJI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA


Monday, October 29, 2012

ule mtandao wa waandishi w ahabari wa mazingira ulioundwa nchini uganda mwaka 2007 kwa ufadhiri wa shirika la SIDA umefia wapi?,ama ndiyo ilikuwa ni njia ya kumalizia fedha za wafadhiri?